فَكَفَرُواْ بِهِۦۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ
Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ulipowajia wao utajo wa watu wa mwanzo na utajo wa watu wa mwisho na kitabu kikamilifu kabisa na bora wa Mitume, naye ni Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, walimkanusha. Basi wataijua adhabu watakayopatiwa Siku ya Mwisho.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس