قَالُواْ لَبِثۡنَا يَوۡمًا أَوۡ بَعۡضَ يَوۡمٖ فَسۡـَٔلِ ٱلۡعَآدِّينَ
Watasema: Tulikaa siku moja au sehemu ya siku. Basi waulize wanao weka hisabu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Watasema kwa kituko cha Kisimamo na ukali wa adhabu, «Tulikuwa huko kwa siku moja au sehemu ya siku. Waulize washika hesabu wenye kuhesabu miezi na siku.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس