قَالَ فِيهَا تَحۡيَوۡنَ وَفِيهَا تَمُوتُونَ وَمِنۡهَا تُخۡرَجُونَ
Akasema: Humo mtaishi, na humo mtakufa, na kutoka humo mtatolewa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mngu, Aliyetukuka, Akasema kumwambia Ādam, Ḥawwā’ na kizazi chao, «Huko ardhini mtaishi, yaani mtapitisha siku za uhai wenu duniani, na huko kitakuwa kifo chenu, na kutoka huko Mola wenu atawatoa na awakusanye mkiwa hai Siku ya Ufufuzi.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس