وَٱلَّذِينَ يُؤۡتُونَ مَآ ءَاتَواْ وَّقُلُوبُهُمۡ وَجِلَةٌ أَنَّهُمۡ إِلَىٰ رَبِّهِمۡ رَٰجِعُونَ
Na wale ambao wanatoa walicho pewa, na hali nyoyo zao zinagopa kwa kuwa watarejea kwa Mola wao Mlezi,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wale wanaojibidiisha kufanya matendo ya kheri na wema, mioyo yao ina kicho cha kuogopa yasikubaliwe matendo yao na yasiwaokoe na adhabu ya Mola wao warejeapo Kwake kwa kuhesabiwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس