وَشَجَرَةٗ تَخۡرُجُ مِن طُورِ سَيۡنَآءَ تَنۢبُتُ بِٱلدُّهۡنِ وَصِبۡغٖ لِّلۡأٓكِلِينَ
Na mti utokao katika mlima wa Sinai, unatoa mafuta na kuwa kitoweo kwa walao.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na tukawatolea nyinyi kwa maji hayo mizaituni ambayo inatoka kandokando ya jabali la Tūr Ṣīnā’ ambao unakamuliwa mafuta ya kujipaka na kutumia kwa chakula.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس