قُل لَّآ أَمۡلِكُ لِنَفۡسِي نَفۡعٗا وَلَا ضَرًّا إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ وَلَوۡ كُنتُ أَعۡلَمُ ٱلۡغَيۡبَ لَٱسۡتَكۡثَرۡتُ مِنَ ٱلۡخَيۡرِ وَمَا مَسَّنِيَ ٱلسُّوٓءُۚ إِنۡ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٞ وَبَشِيرٞ لِّقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ
Sema: Siimilikii nafsi yangu manufaa wala madhara, ila apendavyo Mwenyezi Mungu. Na lau kuwa ninayajua ya ghaibu ninge jizidishia mema mengi, wala ovu lisinge nigusa. Mimi si chochote ila ni mwonyaji na mbashiri kwa watu wanao amini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sema, ewe Mtume, «Siwezi kuiletea mema nafsi yangu wala kuiepushia shari yenye kuifikia, isipokuwa iwapo Mwenyezi Mungu Alitaka. Na lau mimi ningalikuwa najua yaliyofichika ningalifanya njia ambazo najua kwamba zitaniongezea maslahi na manufaa na ningalijikinga na shari yenye kuwa kabla haijatukia. Mimi si yoyote isipokuwa ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Amenituma kwenu, naogopesha mateso Yake na natoa bishara njema ya thawabu Zake kuwalipa watu wanaoamini kuwa mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na wakafuata sheria Yake kivitendo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس