سَآءَ مَثَلًا ٱلۡقَوۡمُ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا وَأَنفُسَهُمۡ كَانُواْ يَظۡلِمُونَ
Huu ni mfano muovu kabisa wa watu wanao kanusha Ishara zetu na wakajidhulumu nafsi zao.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ni mfano mbaya ulioje! Mfano wa watu waliokanusha hoja za Mwenyezi Mungu na dalili Zake wakazikataa na hali kwamba ni nafsi zao wenyewe walikuwa wakizidhulumu kwa sababu ya kukanusha kwao hoja hizi na dalili.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس