وَلَوۡ أَنَّ أَهۡلَ ٱلۡقُرَىٰٓ ءَامَنُواْ وَٱتَّقَوۡاْ لَفَتَحۡنَا عَلَيۡهِم بَرَكَٰتٖ مِّنَ ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِ وَلَٰكِن كَذَّبُواْ فَأَخَذۡنَٰهُم بِمَا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ
Na lau kuwa watu wa miji wangeli amini na wakamchamngu, kwa yakini tungeli wafungulia baraka kutoka mbinguni na katika ardhi. Lakini walikanusha basi tukawapatiliza kwa sababu ya yale waliyo kuwa wakiyachuma.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na lau watu wa miji waliwaamini Mitume wao wakawafuata na kujiepusha na aliyoyakataza Mwenyezi Mungu, Angaliwafungulia Mwenyezi Mungu milango ya heri kwa kila njia. Lakini wao walikanusha, Mwenyezi Mungu Akawatesa kwa adhabu yenye kuangamiza kwa sababu ya ukafiri wao na maasia yao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس