أُبَلِّغُكُمۡ رِسَٰلَٰتِ رَبِّي وَأَنصَحُ لَكُمۡ وَأَعۡلَمُ مِنَ ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ
Nakufikishieni Ujumbe wa Mola Mlezi wangu, na ninakunasihini; na ninayajua kwa Mwenyezi Mungu msiyo yajua nyinyi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Nawafikishia nyinyi lile niliotumwa nalo kutoka kwa Mola wangu, na wapa ushauri kwa kuwaonya na adhabu ya Mwenyezi Mungu na kuwapa bishara njema ya malipo yake mema, na mimi nayajua, kuhusu sheria Yake, msiyoyajua.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس