لَوۡ كَانَ هَـٰٓؤُلَآءِ ءَالِهَةٗ مَّا وَرَدُوهَاۖ وَكُلّٞ فِيهَا خَٰلِدُونَ
Lau kuwa hawa ni miungu, wasingeli ingia. Na wote watadumu humo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Lau hawa ambao mliwaabudu badala ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka walikuwa ni waungu wanaostahiki kuabudiwa, hawangaliingia moto wa Jahanamu pamoja na nyinyi, enyi washirikina. Kwa hakika, wote hao, waabudu na waabudiwa, ni wenye kukaa milele ndani ya moto wa Jahanamu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس