ذَٰلِكَ بِمَا قَدَّمَتۡ أَيۡدِيكُمۡ وَأَنَّ ٱللَّهَ لَيۡسَ بِظَلَّامٖ لِّلۡعَبِيدِ
Haya ni kwa sababu ya iliyo tanguliza mikono yenu, na kwamba Mwenyezi Mungu si mwenye kuwadhulumu waja,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Adhabu hiyo kali ni kwa sababu ya yale mliyoyatanguliza katika maisha yenu ya duniani kati ya maasia ya kimaneno, ya kivitendo na ya kiitikadi, na kwamba Mwenyezi Mungu si Mwenye kuwadhulumu waja Wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس