هُمۡ دَرَجَٰتٌ عِندَ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِمَا يَعۡمَلُونَ
Hao wana vyeo mbali mbali kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona yote wayatendayo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Watu wa Peponi wenye kufuata yenye kumridhisha Mwenyezi Mungu wanatafautiana daraja. Na watu wa Motoni wanaofuata yenye kumkasirisha Mwenyezi Mungu wanatafautiana katika matobwe. Wao hawalingani. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuziona amali zao, hakifichiki chochote Kwake katika matendo yao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس