بَلَىٰۚ مَنۡ أَوۡفَىٰ بِعَهۡدِهِۦ وَٱتَّقَىٰ فَإِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلۡمُتَّقِينَ
Sivyo hivyo, bali anaye timiza ahadi yake na akamchamngu basi Mwenyezi Mungu huwapenda wachamngu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mambo si kama vile walivyodai hawa warongo. Mchaji-Mungu kikweli ni yule aliyetekeleza ahadi aliyomuahidi Mwenyezi Mungu ya kutekeleza amana na kumuamini Yeye na Mitume Wake na akajilazimisha kufuata uongofu Wake na Sharia Yake na akamuogopa Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka, kwa kufuata Aliyoamrisha na kujiepusha na Aliyokataza. Na Mwenyezi Mungu Anawapenda wachamungu wenye kujikinga na ushirikina na maasia.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس