قَالَ رَبِّ ٱجۡعَل لِّيٓ ءَايَةٗۖ قَالَ ءَايَتُكَ أَلَّا تُكَلِّمَ ٱلنَّاسَ ثَلَٰثَةَ أَيَّامٍ إِلَّا رَمۡزٗاۗ وَٱذۡكُر رَّبَّكَ كَثِيرٗا وَسَبِّحۡ بِٱلۡعَشِيِّ وَٱلۡإِبۡكَٰرِ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Niwekee alama. Akasema: Alama yako ni kuwa hutasema na watu kwa siku tatu, isipo kuwa kwa kuashiria tu. Na mdhukuru Mola Mlezi wako kwa wingi na mtakase jioni na asubuhi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Zakariyyā akasema, «Mola wangu, nijaalia alama ambayo itakuwa ni dalili kwangu ya kupata matoto ili nipate kuingiwa na furaha na bashasha.» Akasema, «Alama yako uliyoitaka ni kutoweza kusema na watu kwa siku tatu isipokuwa kwa kuwashiria, pamoja na kuwa wewe uko sawa na mzima. Na katika kipindi hiki, kithirisha kumataja Mola wako na umswaliye katika nyakati za mwisho wa mchana na mwanzo wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس