ٱلَّذِينَ ٱسۡتَجَابُواْ لِلَّهِ وَٱلرَّسُولِ مِنۢ بَعۡدِ مَآ أَصَابَهُمُ ٱلۡقَرۡحُۚ لِلَّذِينَ أَحۡسَنُواْ مِنۡهُمۡ وَٱتَّقَوۡاْ أَجۡرٌ عَظِيمٌ
Walio mwitikia Mwenyezi Mungu na Mtume baada ya kwisha patwa na majaraha - kwa walio fanya wema miongoni mwao na wakamchamngu utakuwa ujira mkubwa -
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wale waliouitikia mwito wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakatoka kuwafuata washirikina mpaka kijiji cha Ḥamrā’ al-Asad baada ya kushindwa katika vita vya Uḥud, pamoja na maumivu na majaraha waliyokuwa nayo, wakafanya upeo wa juhudi zao na wakashikamana na mwongozo wa Mtume wao, basi watenda wema hao na wacha-Mungu hao watapata thawabu kubwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس