أَمۡ حَسِبۡتُمۡ أَن تَدۡخُلُواْ ٱلۡجَنَّةَ وَلَمَّا يَعۡلَمِ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ جَٰهَدُواْ مِنكُمۡ وَيَعۡلَمَ ٱلصَّـٰبِرِينَ
Je! Mnadhani mtaingia Peponi na hali Mwenyezi Mungu hajawapambanua wale miongoni mwenu walio pigana Jihadi, na hajawapambanua walio subiri?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi Maswahaba wa Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie! Kwani mnadhani kwamba mtaingia Peponi na bado hamjapewa mitihani ya vita na mambo mazito? Haitapatikana kwenu kuingia Peponi tu, hivi hivi, mpaka mjaribiwe na Awajuwe Mwenyezi Mungu, ujuzi ulio wazi kwa viumbe, wale wapiganao jihadi kati yenu katika njia Yake na wenye subira ya kupambana na maadui.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس