خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِن نُّطۡفَةٖ فَإِذَا هُوَ خَصِيمٞ مُّبِينٞ
Amemuumba mtu kwa tone la manii. Naye mara amekuwa mshindani dhaahiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Amemuumba binadamu kutokana na maji matwevu, akitahamaki ajiona ana nguvu na majivuno, na akawa mkali wa utesi na kumjadili Mola wake katika kukanusha kufufuliwa na mengineyo, kama vile kusema, «Ni nani atakayeihuisha mifupa iwapo imeoza.» Na akawa ni mwenye kumsahau Mwenyezi Mungu Aliyemuumba kutoka kwenye hali ya kutokuwako.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس