لِّيُنذِرَ مَن كَانَ حَيّٗا وَيَحِقَّ ٱلۡقَوۡلُ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ
Ili imwonye aliye hai, na neno litimie juu ya makafiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
ili imuonye ambaye moyo wake uko hai na akili yake ina nuru, na ili ithibiti adhabu kwa wenye kumkanusha Mwenyezi Mungu, kwa kuwa wao, kwa hii Qur’ani, hoja ya Mwenyezi Mungu ya mkato imewasimamia.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس