رَّبَّنَآ إِنَّنَا سَمِعۡنَا مُنَادِيٗا يُنَادِي لِلۡإِيمَٰنِ أَنۡ ءَامِنُواْ بِرَبِّكُمۡ فَـَٔامَنَّاۚ رَبَّنَا فَٱغۡفِرۡ لَنَا ذُنُوبَنَا وَكَفِّرۡ عَنَّا سَيِّـَٔاتِنَا وَتَوَفَّنَا مَعَ ٱلۡأَبۡرَارِ
Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tumemsikia mwenye kuita akiitia Imani kwamba: Muaminini Mola wenu Mlezi; nasi tukaamini. Basi tusamehe madhambi yetu, na utufutie makosa yetu, na utufishe pamoja na watu wema.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Ewe Mola wetu! Sisi Tumemsikia mlinganizi, naye ni Mtume wako Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, anawaita watu wakuamini Wewe na kukubali Umoja wako na kuzifuata kivitendo Sheria zako, tukauitikia ulinganizi wake na tukauamini utume wake. Basi tusamehe madhambi yetu, uzisitiri aibu zetu na utukutanishe na watu wema.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس