وَلَا تَهِنُواْ وَلَا تَحۡزَنُواْ وَأَنتُمُ ٱلۡأَعۡلَوۡنَ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ
Wala msilegee, wala msihuzunike, kwani nyinyi ndio wa juu mkiwa ni Waumini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wala msidhoofike, enyi Waumini, kupigana na maadui wenu, wala msihuzunike kwa yaliyowapata huko Uhud. Na nyinyi ndio washindi na mwisho mwema ni wenu iwapo mtamuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mtafuata Sheria Zake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس