إِذۡ هَمَّت طَّآئِفَتَانِ مِنكُمۡ أَن تَفۡشَلَا وَٱللَّهُ وَلِيُّهُمَاۗ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ
Makundi mawili miongoni mwenu yakaingiwa na woga kuwa watashindwa - na hali Mwenyezi Mungu ndiye Mlinzi wao; na Waumini wamtegemee Mwenyezi Mungu tu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kumbuka, ewe Mtume, yale mambo yaliyowahusu kina Banū Salimah na Banū Ḥārithah wakati walipowaza kurudi nyuma, wao na kiongozi wao, mnafiki Abdullāh bin Ubayy bin Salūl, kwa kuogopa kukutana na adui. Lakini Mwenyezi Mungu Aliwalinda na Akawahifadhi wakaenda pamoja na wewe wakimtegemea Mwenyezi Mungu. Na kwa Mwenyezi Mungu, Peke Yake, na wajitegemeze Waumini.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس