أَلَمۡ يَرَوۡاْ إِلَى ٱلطَّيۡرِ مُسَخَّرَٰتٖ فِي جَوِّ ٱلسَّمَآءِ مَا يُمۡسِكُهُنَّ إِلَّا ٱللَّهُۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ
Je! Hawawaoni ndege walivyo wat'iifu katika anga la mbingu? Hapana mwenye kuwashika isipo kuwa Mwenyezi Mungu. Hakika katika haya zipo ishara kwa watu wanao amini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Je, hawakutazama washirikina kuwaangalia ndege walivyoendeshwa na kuwezeshwa kuruka angani, baina ya mbingu na ardhi, kwa amri ya Mwenyezi Mungu? Hakuna anaowazuia wasianguke isipokuwa Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, kwa kuwa amewaumbia mbawa na mikia na Akawawezesha kuruka. Hakika katika huko kuendeshwa na kuzuiliwa kuna alama za ushahidi kwa wale wanaoziamini dalili za uweza wa Mwenyezi Mungu
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس