فَأَسۡرِ بِعِبَادِي لَيۡلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Basi enda na waja wangu waliokuamini, wakakusadiki na wakakufuata, ewe Mūsā, katika kipindi cha usiku, kwani nyinyi mtafuatwa na Fir’awn na askari wake. Na nyinyi mtaokolewa, na Fir’awn askari wake watazama.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس