فَٱسۡتَخَفَّ قَوۡمَهُۥ فَأَطَاعُوهُۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَوۡمٗا فَٰسِقِينَ
Basi aliwachezea watu wake, na wakamt'ii. Kwa hakika hao walikuwa watu wapotovu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Fir’awn akazichezea akili za watu wake, akawaita kwenye upotevu na wao wakamtii na wakamkanusha Mūsā. Kwa hakika, wao walikuwa ni watu waliotoka kwenye utiifu wa Mwenyezi Mugu na njia yake ya sawa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس