فَإِذَا قَرَأۡتَ ٱلۡقُرۡءَانَ فَٱسۡتَعِذۡ بِٱللَّهِ مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ ٱلرَّجِيمِ
Na ukisoma Qur'ani mwombe Mwenyezi Mungu akulinde na Shetani maluuni.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na pindi ukitaka, ewe Muumini, kusoma chochote katika Qur’ani, basi jilinde kwa Mwenyezi Mungu na Shari la Shetani aliyefukuzwa kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu kwa kusema, «A'ūdhu bi- Llāhi min ash-Shayttān ar-Rajīm»(Najilinda kwa Mwenyezi Mungu na Shetani Aliyefukuzwa kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu).
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس