وَلَا تَشۡتَرُواْ بِعَهۡدِ ٱللَّهِ ثَمَنٗا قَلِيلًاۚ إِنَّمَا عِندَ ٱللَّهِ هُوَ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
Wala msinunue ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa thamani ndogo. Hakika kilichoko kwa Mwenyezi Mungu ndicho bora kwenu, ikiwa mnajua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wala msivunje ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa kuchukua badala yake kitu kidogo cha starehe ya duniani. Hakika malipo mema yaliyoko kwa Mweneyzi Mungu ya utekelezaji ahadi ni bora kwenu kuliko thamani hii ndogo. Basi iwapo nyinyi ni watu mnaojua, zingatieni tafauti iliyopo baina ya mazuri mawili haya: ya ulimwenguni na ya Akhera.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس