إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ وَٱذۡكُر رَّبَّكَ إِذَا نَسِيتَ وَقُلۡ عَسَىٰٓ أَن يَهۡدِيَنِ رَبِّي لِأَقۡرَبَ مِنۡ هَٰذَا رَشَدٗا
Isipo kuwa Mwenyezi Mungu akipenda. Na mkumbuke Mola wako Mlezi pale unapo sahau, na sema: Asaa Mola wangu Mlezi ataniongoa kwenye uwongozi ulio karibu zaidi kuliko huu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Isipokuwa ufungamanishe neno lako na matakwa ya Mwenyezi Mungu na useme, «Mwenyezi Mungu Atakapo.» Na mkumbuke Mola wako unaposahau kwa kusema, «Mwenyezi Mungu Atakapo.» Na kila unaposahau, mtaje Mwenyezi Mungu, kwani kumtaja Mwenyezi Mungu huondosha kusahau, na useme, «Matarajio ni kwamba Mola wangu Aniongoze njia ya karibu zaidi yenye kufikisha kwenye uongofu na ya sawa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس