وَمَا مَنَعَ ٱلنَّاسَ أَن يُؤۡمِنُوٓاْ إِذۡ جَآءَهُمُ ٱلۡهُدَىٰ وَيَسۡتَغۡفِرُواْ رَبَّهُمۡ إِلَّآ أَن تَأۡتِيَهُمۡ سُنَّةُ ٱلۡأَوَّلِينَ أَوۡ يَأۡتِيَهُمُ ٱلۡعَذَابُ قُبُلٗا
Na hapana kilicho wazuia watu kuamini ulipo wajia uwongofu na wakaomba maghfira kwa Mola wao Mlezi, isipo kuwa yawafikie ya wale wa zamani, au iwafikie adhabu jahara.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hakuna kilichowazuia watu kuamini, alipowajia Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, akiwa na Qur’ani, na kumuomba maghufira Mola wao kwa kutaka Awasamehe, isipokuwa ni kule kushindana kwao na Mtume, kutaka kwao wajiwe na mwendo wa Mwenyezi Mungu wa kuwaangamiza watu waliopita kabla yao au wapatikane na adhabu ya Mwenyezi Mungu waziwazi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس