وَٱلَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمۡوَٰلَهُمۡ رِئَآءَ ٱلنَّاسِ وَلَا يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَلَا بِٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۗ وَمَن يَكُنِ ٱلشَّيۡطَٰنُ لَهُۥ قَرِينٗا فَسَآءَ قَرِينٗا
Na ambao hutoa mali yao kwa kuonyesha watu, wala hawamuamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Mwisho; na yule ambaye Shet'ani amekuwa ndiye rafiki yake, basi ana rafiki mbaya mno.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na pia tumewaandalia adhabu hii wale ambao wanatoa mali yao kwa njia ya ria na kujitangaza na hawamuamini Mwenyezi Mungu, kiitikadi na kivitendo, wala Siku ya Kiyama. Matendo haya mabaya ni miongoni mwa yale yanayolinganiwa na Shetani. Na yoyote yule ambaye Shetani atakuwa ni mwenye kushikamana na yeye, basi mtu mbaya wa kushikamana naye na kufanya naye urafiki ni yeye.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس