إِنِّي وَجَّهۡتُ وَجۡهِيَ لِلَّذِي فَطَرَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ حَنِيفٗاۖ وَمَآ أَنَا۠ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ
Hakika mimi nimeuelekeza uso wangu sawa sawa kwa aliye ziumba mbingu na ardhi, wala mimi si miongoni mwa washirikina.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Mimi nimeelekea kwa uso wangu, katika ibada, kwa Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka, Peke Yake, kwani Yeye Ndiye Aliyeumba mbingu na ardhi, nikiwa kando na ushirikina na nikielekea kwenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu. Na mimi sikuwa ni miongoni mwa wenye kuwashirikisha wengine pamoja na Mwenyezi Mungu.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس