هُوَ ٱلَّذِي خَلَقَكُم مِّن طِينٖ ثُمَّ قَضَىٰٓ أَجَلٗاۖ وَأَجَلٞ مُّسَمًّى عِندَهُۥۖ ثُمَّ أَنتُمۡ تَمۡتَرُونَ
Yeye ndiye aliye kuumbeni kwa udongo, kisha akakuhukumieni ajali, na muda maalumu uko kwake tu. Tena baada ya haya nyinyi mnatia shaka.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Yeye Ndiye Ambaye Alimuumba baba yenu Ādam kutokana na udongo na nyinyi mnatokana na kizazi chake, kisha Akaandika muda wa kusalia kwenu katika uhai huu wa kilimwengu, na Akaandika muda mwingine maalumu hakuna aujuwao isipokuwa Yeye, Aliyetukuka na kuwa juu, nayo ni Siku ya Kiyama. Kisha nyinyi baada ya haya mnashuku juu ya uwezo wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, wa kufufua baada ya kufa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس