ذَٰلِكُمُ ٱللَّهُ رَبُّكُمۡ خَٰلِقُ كُلِّ شَيۡءٖ لَّآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ فَأَنَّىٰ تُؤۡفَكُونَ
Huyo ndiye Mwenyezi Mungu Mola wenu Mlezi, Muumba wa kila kitu. Hapana mungu ila Yeye; basi mnageuzwa wapi?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Yule Aliyewaneemesha neema hizi si mwingine bali ni Mwenyezi Mungu Mola wenu, Muumba vitu vyote. Hapana Mola Anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Yeye. Basi ni vipi nyinyi mnajiepusha na kumuamini Yeye na mnamuabudu asiyekuwa Yeye miongoni mwa masanamu, baada ya kuwafunukia dalili Zake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس