مَّا يَفۡعَلُ ٱللَّهُ بِعَذَابِكُمۡ إِن شَكَرۡتُمۡ وَءَامَنتُمۡۚ وَكَانَ ٱللَّهُ شَاكِرًا عَلِيمٗا
Mwenyezi Mungu hakuadhibuni mkimshukuru na mkamuamini. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kupokea shukrani na ndiye Mwenye kujua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu hatawapa adhabu iwapo nyinyi mumefanya amali njema na mumemuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Kwani Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kila sifa ya upungufu, Hana haja na yoyote asiyekuwa Yeye. Yeye Atawaadhibu waja kwa makosa yao. Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwarudishia shukrani[1] waja Wake kwa utiifu wao Kwake, ni Mjuzi wa kila kitu.
____________________
[1]Maana ya Shākir ikinasibishwa na Mwenyezi Mungu ni «Analipa thawabu nyingi kwa mema machache». Ang. Tafsiri ya Ibn Kathīr Sura:2, aya:158.
____________________
[1]Maana ya Shākir ikinasibishwa na Mwenyezi Mungu ni «Analipa thawabu nyingi kwa mema machache». Ang. Tafsiri ya Ibn Kathīr Sura:2, aya:158.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس