كُلّٗا نُّمِدُّ هَـٰٓؤُلَآءِ وَهَـٰٓؤُلَآءِ مِنۡ عَطَآءِ رَبِّكَۚ وَمَا كَانَ عَطَآءُ رَبِّكَ مَحۡظُورًا
Wote hao tunawakunjulia - hawa na hao - katika neema za Mola wako Mlezi. Wala neema za Mola wako Mlezi hazizuiliki.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kila kundi, miongoni mwa wenye kuufanyia kazi ulimwengu wenye kumalizika na wenye kuifanyia kazi Akhera yenye kusalia, tunalipatia riziki yetu: tunawaruzuku Wauminiu na makafiri ulimwenguni. Kwani riziki inatokana na vipawa vya Mola wako kwa wema Wake; na vipawa vya Mola wako hanyimwi mtu yoyote, awe ni Muumini au ni kafiri.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس