فَلَمَّآ أَن جَآءَ ٱلۡبَشِيرُ أَلۡقَىٰهُ عَلَىٰ وَجۡهِهِۦ فَٱرۡتَدَّ بَصِيرٗاۖ قَالَ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ إِنِّيٓ أَعۡلَمُ مِنَ ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ
Basi alipo fika mbashiri na akaiweka kanzu usoni pake alirejea kuona. Akasema: Je! Sikukwambieni kuwa mimi najua ya Mwenyezi Mungu msiyo yajua nyinyi?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Alipokuja mwenye kumpa bishara Ya’qūb kwamba Yūsuf yuko hai, akaitupa kanzu ya Yūsuf usoni mwake akarudi Ya’qūb kuwa yuaona, akajawa na furaha na akawaambia waliokuwa hapo kwake, «Je, sikuwapa habari kwamba mimi nayajua kutoka kwa Mwenyezi Mungu msiyoyajua ya fadhila Zake, rehema Zake na ukarimu Wake.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس