قَالَ لَنۡ أُرۡسِلَهُۥ مَعَكُمۡ حَتَّىٰ تُؤۡتُونِ مَوۡثِقٗا مِّنَ ٱللَّهِ لَتَأۡتُنَّنِي بِهِۦٓ إِلَّآ أَن يُحَاطَ بِكُمۡۖ فَلَمَّآ ءَاتَوۡهُ مَوۡثِقَهُمۡ قَالَ ٱللَّهُ عَلَىٰ مَا نَقُولُ وَكِيلٞ
Akasema: Sitampeleka nanyi mpaka mnipe ahadi kwa Mwenyezi Mungu kwamba lazima mtamrejeza kwangu, ila ikiwa mmezungukwa. Basi walipo mpa ahadi yao alisema: Mwenyezi Mungu ndiye Mtegemewa kwa tuyasemayo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ya’qūb, amani imshukiye, akasema kuwaambia, «Sitamuacha aende na nyinyi mpaka mchukue ahadi na mniapie kwa Mwenyezi Mungu kwamba mtamrudisha kwangu, isipokuwa iwapo mtashindwa nguvu msiweze kumuokoa. Basi walipompa ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa lile alilolitaka, Ya’qūb alisema, «Mwenyezi Mungu kwa tunalolinena Ndiye mtegemewa» Yaani, ushahidi Wake kwetu na utunzi Wake zinatutosha.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس