قَالَ رَبِّ ٱلسِّجۡنُ أَحَبُّ إِلَيَّ مِمَّا يَدۡعُونَنِيٓ إِلَيۡهِۖ وَإِلَّا تَصۡرِفۡ عَنِّي كَيۡدَهُنَّ أَصۡبُ إِلَيۡهِنَّ وَأَكُن مِّنَ ٱلۡجَٰهِلِينَ
Yusuf akasema: Ee Mola Mlezi wangu! Nastahabu kifungo kuliko haya anayo niitia. Na usipo niondoshea vitimbi vya wanawake mimi nitamili kwao, na nitakuwa katika wajinga.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Yūsuf akasema, akijilinda na shari lao na vitimbi vyao, «Ewe Mola wangu! Jela ni bora kwangu kuliko yale wanayoniitia ya kufanya machafu. Na usiponiepulia vitimbi vyao, nitalemea kwao na nitakuwa ni miongoni mwa wachache wa akili wenye kujifanyia madhambi kwa ujinga wao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس