يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَقُولُواْ قَوۡلٗا سَدِيدٗا
Enyi mlio amini! Mcheni Mwenyezi Mungu na semeni maneno ya sawasawa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkazifuata Sheria Zake kivitendo, fanyeni matendo ya kumtii na mjiepushe na matendo ya kumuasi, ili msistahili kupata mateso hayo. Na semeni, katika hali zenu zote na mambo yenu yote, maneno ya kunyoka na yanayolingana na usawa, yasiyokuwa na urongo na ubatilifu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس