وَلَا تَكُونَنَّ مِنَ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ فَتَكُونَ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ
Na kabisa usiwe miongoni mwa wale wanao zikanusha Ishara za Mwenyezi Mungu, usije kuwa katika walio khasiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na usiwe, wala usiwe, ewe Mtume, ni miongoni mwa waliokanusha hoja za Mwenyezi Mungu na dalili Zake, ukawa ni katika waliopata hasara ambao Mwenyezi Mungu Amewakasirikia na wamepata mateso Yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس