أَلَآ إِنَّ لِلَّهِ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَن فِي ٱلۡأَرۡضِۗ وَمَا يَتَّبِعُ ٱلَّذِينَ يَدۡعُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ شُرَكَآءَۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَإِنۡ هُمۡ إِلَّا يَخۡرُصُونَ
Jueni kuwa ni vya Mwenyezi Mungu vyote viliomo mbinguni na ardhinii. Na wala hawawafuati hao wanao waomba badala ya Mwenyezi Mungu kuwa ni washirika wake. Wao hawafuati ila dhana tu, na hawasemi ila uwongo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Jueni mtanabahi kwamba ni wa Mwenyezi Mungu kila aliye mbinguni au ardhini miongoni mwa Malaika, binadamu, majini na wengineo. Na ni nini wanachofuata wale wanaowaomba asiyekuwa Mwenyezi Mungu katika hao washirika? Hawana wanachokifuata isipokuwa shaka, na wao hawana lolote isipokuwa wanasema urongo katika yale ambayo wanamnasibisha nayo Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس