وَلَن يَتَمَنَّوۡهُ أَبَدَۢا بِمَا قَدَّمَتۡ أَيۡدِيهِمۡۚ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلظَّـٰلِمِينَ
Wala hawatayatamani kamwe kwa sababu ya yale yaliyo tangulizwa na mikono yao; na Mwenyezi Mungu ni mwenye kuwajua vyema wanao dhulumu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hawatalifanya hilo kabisa, kwa wanayoyajua ya ukweli wa Nabii Muhammad, rehema na amani zimshukie, na ya urongo na uzushi wao, na kwa ukafiri na uasi walioufanya unaopelekea kukoseshwa Pepo na kuingia Motoni. Na Mwenyezi Mungu Anawajua madhalimu miongoni mwa waja wake na Atawalipa kwa dhulma zao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس