ثُمَّ قِيلَ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ ذُوقُواْ عَذَابَ ٱلۡخُلۡدِ هَلۡ تُجۡزَوۡنَ إِلَّا بِمَا كُنتُمۡ تَكۡسِبُونَ
Kisha walio dhulumu wataambiwa: Onjeni adhabu ya kudumu. Kwani mtalipwa isipo kuwa yale mliyo kuwa mkiyachuma?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kisha wataambiwa waliozidhulumu nafsi zao kwa kumkanusha kwao Mwenyezi Mungu, «Onjeni adhabu ya Mwenyezi Mungu ya daima milele kwenu, kwani mnateswa isipokuwa ni kwa yale matendo ya kumuasi Mwenyezi Mungu mliokuwa mkiyafanya katika maisha yenu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس