إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ وَأَقَامُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتَوُاْ ٱلزَّكَوٰةَ لَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ وَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ
Hakika wale walio amini na wakatenda mema na wakashika Sala na wakatoa Zaka, wao watapata ujira wao kwa Mola wao Mlezi, wala haitakuwa khofu juu yao, wala hawatahuzunika.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakatenda matendo mema, wakatekeleza Swala kama Alivyoamrisha Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakatoa Zaka za mali yao, wana thawabu kubwa zinazowahusu wao mbele ya Mola wao na Mruzuku wao. Na hawatapatwa na woga katika Akhera yao, wala masikitiko juu ya mambo mazuri ya kilimwengu waliyoyakosa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس