۞يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلۡخَمۡرِ وَٱلۡمَيۡسِرِۖ قُلۡ فِيهِمَآ إِثۡمٞ كَبِيرٞ وَمَنَٰفِعُ لِلنَّاسِ وَإِثۡمُهُمَآ أَكۡبَرُ مِن نَّفۡعِهِمَاۗ وَيَسۡـَٔلُونَكَ مَاذَا يُنفِقُونَۖ قُلِ ٱلۡعَفۡوَۗ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ ٱللَّهُ لَكُمُ ٱلۡأٓيَٰتِ لَعَلَّكُمۡ تَتَفَكَّرُونَ
Wanakuuliza juu ya ulevi na kamari. Sema: Katika hivyo zipo dhambi kubwa na manufaa kwa watu. Lakini dhambi zake ni kubwa zaidi kuliko manufaa yake. Na wanakuuliza watoe nini? Sema: Kilicho chepesi. Namna hivi Mwenyezi Mungu anakubainishieni Aya zake mpate kufikiri--
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wanakuuliza Waislamu, ewe Nabii, hukumu ya kutumia khamr kwa kunywa, kuuza na kununua. Khamr ni kila chenye kulewesha kinachofinika akili na kuziba, kiwe ni chenye kunywewa au kuliwa. Na wanakuuliza kuhusu hukumu ya kamari. Kamari ni kupokea au kutoa mali kwa bahati nasibu, nayo ni mashindano ambayo yana kupeana badali kutoka pande mbili za ushindani. Waambie, «Katika hayo pana madhara mengi na uharibifu mwingi katika dini na dunia, na akili na mali. Na yamo, katika mambo mawili hayo, manufaa kwa watu, kwa upande wa kuchuma mali na mengineyo. Na madhambi yake ni makubwa zaidi kuliko manufaa yake, kwani huzuia kumtaja Mwenyezi Mungu na kusali, na yote mawili yanaleta uadui na kuchukiana kati ya watu na yanaharibu mali. Huu ulikuwa ni utayarishaji wa kuyaharamisha mambo mawili hayo. Na wanakuuliza kuhusu kiwango ambacho wao wakitoe katika mali yao kwa njia ya sadaka na kujitolea.Waambie, «Toeni kiwango kinachozidi baada ya mahitaji yenu.» Mfano wa haya maelezo yaliyo wazi, Mwenyezi Mungu Anawabainishia aya na hukumu za Sheria, ili mpate kuyafikiria yenye manufaa kwenu
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس