يَدۡعُواْ مِن دُونِ ٱللَّهِ مَا لَا يَضُرُّهُۥ وَمَا لَا يَنفَعُهُۥۚ ذَٰلِكَ هُوَ ٱلضَّلَٰلُ ٱلۡبَعِيدُ
Badala ya Mwenyezi Mungu, yeye huomba kisicho mdhuru wala kumnufaisha. Huko ndiko kupotolea mbali!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Huyo aliyepata hasara anakiabudu kitu, badala ya Mwenyezi Mungu, kisichomdhuru lau akikiwacha wala kumnufaisha akikiabudu. Huko ndiko kupotea kulioko mbali na haki.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس