فَقَدۡ كَذَّبُوكُم بِمَا تَقُولُونَ فَمَا تَسۡتَطِيعُونَ صَرۡفٗا وَلَا نَصۡرٗاۚ وَمَن يَظۡلِم مِّنكُمۡ نُذِقۡهُ عَذَابٗا كَبِيرٗا
Basi walikukanusheni kwa mliyo yasema. Kwa hivyo hamwezi kujiondolea wala kujisaidia. Na atakaye dhulumu miongoni mwenu tutamwonjesha adhabu kubwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hapo waambiwe washirikina, «Kwa kweli, wamewakanusha nyinyi, hawa mliowaabudu kwenye madai yenu juu yao. Enyi hawa, nyinyi hamuwezi kuzikinga nafsi zenu na adhabu wala kuziokoa. Na mwenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu, akajidhulumu nafsi yake, akamuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu na akafa katika hali hiyo, mwenyezi Mungu Atamuadhibu adhabu kali.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس