إِلَّا مَن تَابَ وَءَامَنَ وَعَمِلَ عَمَلٗا صَٰلِحٗا فَأُوْلَـٰٓئِكَ يُبَدِّلُ ٱللَّهُ سَيِّـَٔاتِهِمۡ حَسَنَٰتٖۗ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورٗا رَّحِيمٗا
Isipo kuwa atakaye tubu, na akaamini, na akatenda vitendo vyema. Basi hao Mwenyezi Mungu atayabadilisha maovu yao yawe mema. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Lakini mwenye kutubia kutokana na madhambi haya toba ya dhati na akaamini imani ya kukata yenye kuambatana na matendo mema, basi hao Mwenyezi Mungu Atawafutia makosa yao na Atawaweka mahali Pake mema, kwa sababu ya kutubia kwao na kujuta kwao. Na kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe kwa anayetubia, ni Mwingi wa rehema kwa waja Wake kwa kuwa Amewaita watubie baada ya kushindana na Yeye kwa kufanya maasia makubwa kabisa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس