۞وَهُوَ ٱلَّذِي مَرَجَ ٱلۡبَحۡرَيۡنِ هَٰذَا عَذۡبٞ فُرَاتٞ وَهَٰذَا مِلۡحٌ أُجَاجٞ وَجَعَلَ بَيۡنَهُمَا بَرۡزَخٗا وَحِجۡرٗا مَّحۡجُورٗا
Naye ndiye aliye zipeleka bahari mbili, hii tamu mno, na hii ya chumvi chungu. Na akaweka baina yao kinga na kizuizi kizuiacho.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Mwenyezi Mungu Ndiye Aliyezichanganya bahari mbili: ya tamu yenye ladha nzuri, na ya chumvi yenye uchumvi mwingi, na Akaweka baina ya hizo mbili kizuizi chenye kuzuia kila mojawapo ya hizo isiiharibu nyingine na pingamizi ili mojawapo isiifikie nyingine.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس