أَمۡ يَقُولُونَ ٱفۡتَرَىٰهُۖ قُلۡ إِنِ ٱفۡتَرَيۡتُهُۥ فَعَلَيَّ إِجۡرَامِي وَأَنَا۠ بَرِيٓءٞ مِّمَّا تُجۡرِمُونَ
Au ndio wanasema: Ameizua? Sema: Ikiwa nimeizua, basi kosa hilo ni juu yangu, na mimi sikhusiki na makosa myatendayo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Au je, wanasema hawa washirikina miongoni mwa watu wa Nūḥ, kwamba Nūḥ, amezua neno hili? Waambie, «Nikiwa nimemzulia urongo Mwenyezi Mungu hilo, basi ni juu yangu mimi, peke yangu, dhambi ya hilo; na nikiwa ni mkweli, basi nyinyi ndio wahalifu wenye dhambi, na mimi niko mbali na ukfiri wenu, ukanushaji wenu uhalifu wenu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس