وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوۡمِهِۦٓ إِنِّي لَكُمۡ نَذِيرٞ مُّبِينٌ
Na Sisi tulimtuma Nuhu kwa watu wake, akawaambia: Hakika mimi ni mwonyaji kwenu ninaye bainisha,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika tulimtuma Nūḥ, kwa watu wake akasema kuwaambia, «Mimi ni muonyaji kwenu adhabu ya Mwenyezi Mungu, ni mwenye kuwabainishia yale niliyotumwa kwenu ya maamrisho ya Mwenyezi Mungu na makatazo yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس